WIZARA ZAASI SERIKALI

Wizara ya maswala ya ndani ya Libya imetoa taarifa ikisema kuwa inaunga mkono kampeini dhidi ya serikali inayoongozwa na jenerali wa zamani wa jeshi la taifa aliyeasi serikali tawala.


Hata hivyo waziri husika Salihal-Mazig baadaye alikanusha kumuunga mkono jenerali muasi Khalifa Haftar, aliyeanzisha operesheni ijumaa iliyopita.

Jenerali Haftar amezindua kampeini ya kivita inayolenga kuing'oa mamlakani utawala uliomrithi aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo Maummar Gaddafi kuanzia kwa bunge lililoshambuliwa siku ya jumapili.

Jenerali huyo aliongoza wapiganaji wake kuvamia mjiwa Benghazi katika kampeini anayoiita "Libya's Dignity".


Jenerali huyo anailaumu serikali kwa kuwatepetevu dhidi ya wapiganaji waasi.Wizara ya maswala ya ndani tayari imemuunga mkono katika mtandao wake wa kijamii wa Facebook.

Jumatatu hii kiongozi wa jeshi la wanahewa la Libya Jenerali Guma al-Abany, alitoa ujumbe wa kumuunga mkono Jenerali huyo aliyestaafu akisema hatua yake ni jambo la kupigiwa mfano kwa walibya wazalendo.

Kiongozi wa jeshi la wanamaji Brigadia jenerali Hassan Abu-Shannaq, alinusurika jaribio la mauaji muda mchache tu baada ya kutangaza kumuunga mkono jenerali huyo aliyezindua vita dhidi ya wapiganaji wakiislamu ambao wanalumiwa kwa utovu wa usalama nchini Libya.


Serikali imempuzilia mbali jenerali Khalifa Haftar na ikasema kuwa haita jiuzulu.

Takriban watu 100 wameripotiwa kuuawa tangu mapigano hayo kuzuka ijumaa iliyopita na kuilazimisha serikali kuitisha uchaguzi wa haraka tarehe 25 mwezi juni.

Iwapo uchaguzi huu utaendelea mbele basi utakuwa ni uchaguzi wa pili tangu aliyekuwa rais Muammar Gaddafi kungolewa madarakani mwaka wa 2011.

Hadi kufikia sasa Libya imekuwa na mawaziri wakuu watatu tangu mwezi Machi mwaka huu.