WALIO MUUA DEREVA BODABODA SAMWELI KUFIKISHWA MAHAKAMANI(Tunaomba Radhi kwa muonekano wa picha)

(Picha ni majambazi waliokamatwa kuhusiana na tukio hilo).

Jeshi la Polisi Wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kumuuwa Bodaboda mmoja aitwaye Frenk Joseph (25)mkazi wa mtaa wa Nsemlwa Wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi kwa kumchinjashigo na kisha kumpola pikipiki yake aina ya SANLG yenye namba za usajiri T 704 CDQ Kamanda wa jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi
Kamishina msaidizi mwandamizi Dhahiri Kidavashari aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Charles Kidaha(29),Madia Mtema (40) na Buyenza Jendesha (40) wote wakazi waTarafa ya Mwese Wilayani Mpanda.

Kidavashari alisema watuhumiwa hao walimuuwa bodaboda huyo hapo Aprili 26 mwaka huu majira ya saa saa kumi na moja jioni huko katika eneo la Kijiji cha Mpembe Tarafa ya Mwese Wilayani Mpanda.

Siku hiyo ya tukio marehemu Samwel alikuwa kwenye kijiwe chake cha Bodaboda kilichoko kwenye hospitali ya Wilaya ya Mpanda akiwa na pikipiki yake aina ya Sunlg yenye Namba za usajiri T704CDQ aAlisema wakati akiwa kwenye kituo hicho cha Bodaboda alitokea mtu asiye fahamika na kumkodisha marehemu ambapo waliondoka nae huku marehemu akiwa aja waaga bodaboda na kuwafahamisha mahari alikokuwa wakielekea na mteja wake huyo.

Alifafanua kuwa ndipo siku iliyofuata ya tarehe 27 Aprili mwili wa marehemu bodaboda huyo ulipoonekana ukiwa umetelekezwa porini katika kijiji cha Mpembe huku akiwa amechinjwa na kitu chenye ncha kali na pikipiki yake haikuonekana katika eneo hilo.

Kamanda Kidavashari alieleza kuwa baada ya tukiola mauwaji hayo polisi waliendelea kufutilia tukio hilokwa kushirikiana na raia wema na ndipo hapo mei 22 majira ya saa kumi na moja jioni huko katika kijiji cha Kasekese Kata ya Simbwesa Wilaya ya Mpanda raia wemawalitowa taarifa kwa jeshi la polisi kuwa wanamashaka na watuhumiwa hao kwani waliwasili kijijni hapo wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki moja.

Alisema baada ya taarifa hizo jeshi la polisi liliweza kufanikiwa kufika kijijini hapo mara tuu baada ya muda mfupi na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wote watatu wakiwa na pikipiki hiyo ya marehemu Samweli waliompola baada ya kumuuwa.

Katika maojiano ya awali bainiya jeshi la polisi na watuhumiwa hao watatu imeonyesha kuwa watuhumiwa hao ndio waliohusika na mauwaji ya bodaboda huyo.

Kamanda Kidavashari ameleza watuhumiwa hao wote watatu wanatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamiliki.
Picha jinsi alivyochinjwa)