MAMA NA MWANAE WAUAWA KWA KUPIGWA RISASI

Mwanamke ajulikanaye kwa jina la Milembe Masanja na mtoto wake aitwaye Kulwa Madirisha wakazi wa kijiji cha Nyabusalu wilayani Kahama, wameuwawa kwa kupigwa risasi saa 2 usiku, wakati wakiandaa chakula.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Evarist Mangalla amesea Milembea aliuwawa kwa kupigwa risasi kwenye kwapa la kushoto huku mwanaye Kulwa akipigwa risasikidevuni na tumboni, hali iliyosababisha vifo vyao papo hapo.

Hadi sasa chanzo cha tukio kinachunguzwa na hakuna mtu anayeshikiliwa.

Kamanda Mangalla pia amesema bunduki ni aina ya gobore kutokana na majeraha waliyokutwa nayo marehemu.