UNAFIKI WA WABUNGE WA CHADEMA LISSU, MSIGWA, LEMA WAJULIKANA WAPOKEA HONGO TOKA KWA MUHONGO

KASHFA KUBWA YA RUSHWA WABUNGE WA CHADEMA MUHONGO AWAHONGA MAMILLIONI ILI KUPITISHA HOTUBA YAKE LISSU, MSIGWA NA LEMA WACHUKUA MAMILIONI HAYO, WAMTOSA SUGU SUGU AGOMA KUSOMA SHUTUMA DHIDI YA ZITTO KWA SABABU YA KUNYIMWA GANJI.

Hali inayoendelea hivi sasa ni hatarikwa ustawi wa Upinzani wa kweli na uhakika hapa nchini kiasi cha wabunge wenzangu CHADEMA kukubali kupokea Rushwa ili waweze kumkashifu na kumchafua mbunge mwenzao Zitto Zuberi Kabwe. Hali hii imejitokeza rasmi kwa kipindi cha wiki nzima sasa hasakuelekea kupitishwa kwa bajeti ya wizara ya nishati na madini. Mkakati mzima upo kama ifuatavyo na kwa sasa ninaufichua kwa siri lakini muda si mrefu nitausema hadharani ili kila mtu ajue hasa nini kinaendelea.

MKAKATI ULIVYO

Juzi Jumaatatu usiku Wabunge wa CHADEMA ikiwa ni pamoja na MIMI,TUNDU LISSU PETER MSIGWA na GODBLESS LEMA tulikutana na katibu mkuu wa wizara ya nishati namadini ndugu ELIAKIM MASWI , na waziri wake PROF. MUHONGO kwa nyakati tofauti tofauti zaidi ya mara moja na kila mmoja kwa wakati wake.

Katika makutano hayo MASWI na MUHONGO wametuomba sisi WABUNGE WA CHADEMA kuhakikisha tunawafunga midomo wabunge wote makini ili waweze kupitisha kwa urahisi bajeti yao.

Katika mikutano huo uliofanyika katika hotel za ST. GASPER, Dodoma Hotel na Royal Village, kwa pamoja tulikubaliana kuhakikisha tunamshambulia ZITTO KABWE hasakwa madai makuu mawili 1. Kwamba yeye ndio kiongozi mkuu wa kujidai anatetea maslahi ya wanyonge na kwamba anawatumia wabunge kina KAFULILA na wengine kwenye sakata la IPTL ambalo linaonyesha kuinyima usingizi WIZARA kutokana na UFISADI wa zaidi ya BILLIONI 200. 2. Kwamba wamepata documents zinazomuhusisha zitto na matumizi mabaya ya madaraka. Ndio maana wanaanza nae na kwamba yeye si msafi kama anavyojifanya.


MAKUBALIANO

Tumeahidiwa kila mmoja kupewa MILLIONI 10 kama suala hili litakamilika ipasavyo, na Tayari tumeshachukua kila mmoja shilingi MILLIONI 5 . nitakapochangia BUNGENI NITAWEKA WAZI KILA KITU


SUGU AWAKATALIA

Mbunge mwenzetu JOSEPH MBILINYI-SUGU mbaye ni Waziri Kivuli wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo ameingizwa Mkenge kwa kujikuta akishindwa kuzisoma PARAGRAPH zilizoingizwa kinyemela na wenzake hao waliokula mlungula na Badala yake kuziruka.

Ilikuwa hivi, mchungaji msigwa alimfuata SUGU na kumuambia akasome kipengele kinachomuonyesha zitto kabwe kutumia vibaya madaraka yake, SUGU akakubali, lakini baadae alipogundua kama wenzake wameramba mlungula akawagomea, kwa kuwa aliyeiandaa hotuba ya SUGU ni LISSU, basi akaiandika kwa siri, lakini SUGU alipokuwa anasoma akagundua kwamba imepenezwa tena, SUGU AKAAMUA KURUKA KIPENHELE HICHO. NDIO MAANA SUGU HAKUONEKANA AKISOMA SEHEMU HIYO. LAKINI KWA KUWA KINA LISSU WALISHAKULA HELA ZA MOTO IKABIDI WACHUKUE SEHEMUYA HANSARD NA KUISAMBAZA MITANDAONI KWAMBA SUGU AMLIPUA ZITTO KABWE, ILI WASIONEKANA WAONGO. KWA KINA MASWI NA MUHONGO.

MBUNGE DAVID SILINDE yeye alikataa kabisa kuwa sehemu ya UNAFIKI HUU WA KISIASA.


KAZI INAYOFUATA,.

Kuanzia tarehe 30.5.2014, wabunge MSIGWA, LEMA na LISSU wataanza kuchangia kwa kumshambulia ZITTO KABWE katika kile wanachokiita kumshuhulikia, lakini hii ni kwamba watakuwa wanatii Makubaliano yao na MUHONGO NA MASWI.

MSIGWA ATAMSHAMBULIA ZITTO KABWE LISSU AYAMSHAMBULIA ZITTO KABWE LEMA ATAMSHAMBULIA Na Tumeagizwa KURUDISHA Hongo Hizo ikiwa hawatawashambulia..


UZOEFU UKOJE

Kila kinapofika kipindi cha WIZARA YA NISHATI NA MADINI kusoma BAJETI YAKE huzushwa shutuma kalidhidi ya WABUNGE MAKINI WENYE KUHOJI MASWALA YA MSINGI KWA TAIFA. 1. MWAKA 2012 LISSU, MSIGWA, LEMA na NASSARY walimshutumu ZITTO KABWE kuhongwa na MKURUGENZI WA TANESCO, lakini ilipoundwa Tume Kuchunguza wakagundulika kuwa walitumika KISIASA kumchafua ZITTO na kwamba habari zile hazikuwa sahihi. 2. MWAKA huu wanafanya mchezo ule ule.

Nitaendelea kutoa ushirikiano kwa WAZALENDO wenzangu kwa kadri itakavyohitajika.

Na ninampongeza KAMANDA SUGU kwa kitendo chakecha kishujaa cha kukataa kumezeshwa maneno asiyoyaamini yaliyotokana na Rushwa iliyotolewa kwetu mimi, MSIGWA, LEMA na LISSU.

Pakua hapa -----> http://ubuntuone.com/3Yvcq8P9kqiHBUtIcCzFB5