UKAWA WAANZA ZIARA YA SIKU 10 BARA

Wakati Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), ukitarajiwa kuanza ziara ya siku 10 katika mikoa ya Tanzania Bara kesho, viongozi wa umoja huo wamemvaa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwa kauli yake kuwa Katiba haina umuhimu.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema jana kwamba ameshangazwa na kauli ya Kinana kwa kuifananisha Tanzania na Uingereza ambayo haina Katiba.

"Kauli hii imenipa matatizo, naanza kutilia shaka kisomo cha hawa wenzetu..."

Hawana Katiba ya kuandika lakini wana sheria zao ambazo wanaziheshimu, ndiyo maana huwezi kuwahoji kuhusu Malkia Elizabeth wakakuelewa.


Mikutano ya Ukawa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro alisema awamu ya kwanza ya ziara hiyo itaanza kesho hadi Mei 26, mwaka huu.

Alisema ili kufanikisha ziara hiyo, Ukawa imejigawa katika timu tatu ambazo zitakuwa zinafanya mikutano na maandamano ya amani.


Kundi la kwanza litaongozwa na Katibu Mkuu wa NCCR- Mageuzi, Mosena Nyambabe, la pili litakuwa na Dk Slaa na la tatu litakuwa chini ya Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba.