ZAIDI YA WATU 2000 WAHOFIWA KUFA

Watu zaidi ya 2,500 wanahofiwa kufariki dunia baada ya kufukiwa na mmomonyoko wa ardhi Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo katika Jimbo la Badakhshan.

Taarifa nyingine zilizotolewa na Umoja wa Mataifa (UN), zinaeleza kwamba zaidi ya miili 350 imepatikana katika jimbo hilo.


Katika eneo hilo maelfu ya makazi ya watu yamefukiwa na matope baada ya mlima katika jimbo hilo kuporomoka kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.
Polisi wamekuwa wakiwapelekea mikate na maji raia walionusurika kwa kuwa usiku wa Ijumaa kuamkiajana, walishinda bila chakula. Mvua kubwa zimekuwa zikinyesha kwa wingi Kaskazini na Mashariki mwa Afghanistan na kusababisha madhara hayo.


"Idadi ya watu waliofariki dunia imefikia 350 na nyumba zaidi ya 1,000 zimearibiwa na mvua," taarifa ya UN ilieleza.

Taarifa ya UN ilieleza kwamba zaidiya nyumba nyingine 300, zimefukiwa baada mlima kwenye jimbo hilo kuporomoka.


Kamanda wa Polisi katika Jimbo la Badakhshan, Fazludeen Ayaz alisema katika Kijiji cha Hargu, nyumba za familia 215 zilifunikwa na udongo.

Ayaz alisema endapo kuna watu wamenusurika katika ajali hiyo itakuwa vigumu kuwaokoa kutokanana kufunikwa na matope.


Jimbo la Badakhshan linatajwa kuwa wanaishi watu wa kipato cha chini mpakani mwa Tajikistan, China na Pakistan.