MAREKANI KUSAIDIA NIGERIA KUTAFUTA MATEKA

Marekani imetangaza kwamba imetuma kikosi cha wataalamu nchini Nigeria kusaidia kuwatafuta wasichana takriban 200 wa shule waliotekwa nyara mwezi uliopita na wapiganaji wa kundi la Boko Haram.


Rais Barack Obama ameshutumu utekaji nyara wa wasichana hao na kusemakuwa mataifa yanapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kulikomesha Boko Haram."Tayari tumetuma kundi letu Nigeria.

Wamekubali msaada wetu ambao unashirikisha wanajeshi, wadumishaji wa sheria na mashirika mengine ambao wanajaribu kutambua waliko wasichana hawa ili wawape msaada," Rais Obama alisema.

Rais Obama amesema kuwa jamii ya kimataifa inapaswa kutumia utekeji wa kikatili wawasichana hao kama msingi wa kuungana na kuangamiza Boko Haram.


Nchini Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amekubalimsaada huo kama alivyosema msemaji wake, Daktari Reuben Abati.

"Msaada huo kutoka kwa Rais Obama uliwasilishwa na Waziri wa Mashauri ya Kigeni John Kerry kama saa tisa alasiri hivi," Daktari Abati alisema.