ISRAEL YASAIDIA NIGERIA KUTAFUTA WASICHANA

Kikosi cha Israel cha kukabiliana na ugaidi kinatarajiwa kujiunga na juhudi za kuwatafuta zaidi ya wasichana 200 waliotekwa nyara nchini Nigeria na wanamgambo wa kundi la Boko Haram.


Kundi hilo litajiunga na wataalamu wa Marekani,Uingereza na ufaransa ambao tayari wako nchini Nigeria.

Rais Goodluck Jonathan amesema kuwa kujiunga kwa Israel katika operesheni hiyo ni wazi kwamba dunia nzima inaunga mkono usakaji wa wasichana hao.


Mwandishi wa BBC nchini Nigeria amesema kuwa uwepo wa wataalam wa Israel katika oparesheni hiyo huenda kukazua hisia za kisiasa nchini Nigeria ambapo wasiwasi kati ya wakristo wanaoshi kusini mwa taifa hilo na waislamu wanaoishi kazkazini huzua ghasia.

Awali Gavana wa jimbo la Borno Kaskazini Mashariki mwa taifa hilo, eneo ambalo wasichana hao walitekwanyara alisema kuwa ana habari kuhusu kule walipo wasichana hao.