TANZANIA YAPOTEZA SH 3 TRILION ZA KODI

Utafiti mpya umebaini kuwa Tanzania inapoteza zaidi ya Sh3 trilioni kila mwaka kutokana na ukwepaji kodi unaofanywa na kampuni za uchimbaji madini na katika uingizaji bidhaa na kuuza nje.


Shirika la kiuchumi lenye makazi yake Marekani (GFI), lilitoa ripoti yake mwishoni mwa wiki iliyopita likieleza kuwa Tanzania inaongoza kwa kupoteza fedha nyingi zaidi kutokana na udanganyifu huo miongoni mwa nchi tano zilizofanyiwa utafiti za Kenya, Uganda, Ghana na Msumbiji.

Kiasi cha fedha kinachopotea kila mwaka, kingeweza kujenga zahanati 374 za kisasa kwa Sh8.1 bilioni kila moja.


Vilevile, utafiti huo umeonyesha kuwa kiasi hicho kinachopotea kingeweza kulisaidia Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuzalisha nishati ya kiasi cha megawati 1,800, tatizo ambalo limekuwa sugu kwa miongo mingi.

Pia, kiasi hicho kingeliwezesha Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kununua ndege 30 aina ya A320 ambayo hugharimu dola 60 milionikila moja.
Hivi karibuni Shirika la Ndege la Afrika Kusini lilinunua ndege hiyo.


Udanganyifu katika mauzo ulionekana zaidi katika uingizaji mafuta yenye msamaha wa kodi kwa kampuni za madini.

Ripoti hiyo inaonyesha kuwa huenda kampuni za madini hupandisha gharama za uingizaji wanishati hiyo ili kuhamisha fedha njeya nchi kwa njia haramu.


Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kiwangoambacho Tanzania hupoteza kila mwaka ni sawa na asilimia 16 ya bajeti ya sasa.

Utafiti huo pia unaonyesha kuwa kiasi kinachopotea ni mara tatu ya kile ambacho Serikali ilitangaza kukopa kupitia mashirika ya mikopo yenye masharti nafuu katika bajeti yake ya sasa.


Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Tanzania inafuatiwa na Kenya ambayo inapoteza Sh131 bilioni za Kenya (Sh2.489 trilioni), Ghana Dola za Marekani 1.44 bilioni (Sh2.304 trilioni) na Uganda Sh2.2 trilioni za Uganda (Sh1.4 trilioni) na Msumbiji iliyopoteza Dola za Marekani 585