BOKO HARAM WAFANYA SHAMBULIZI

Taarifa kutoka nchini Nigeria, zinasema kuwa mamia ya watu waliuawa katika shambulizi lililofanywa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram katika mpaka wa nchi hiyo na Cameroon siku ya Jumanne.


Katika mahojiano na BBC kiongozi mmoja wa eneo hilo, Ahmed Zanna, alisema kuwa washukiwa walivamia mji wa Gamboru Ngala, katika jimbo la Borno, na kuwaua takriban watu 300.

Inaarifiwa wapiganaji hao waliwafyatulia risasi watu kiholela katika soko kuu la eneo hilo.


Mwandishi wa BBC nchini Nigeria anasema ilikuwa vigumu kupata taarifa hizo mapema kwa sababu ya changamoto ya mawasiliano katika jimbo hilo hasa kwa sababu eneo hilo liko mbali sana.

Wakazi wa eneo hilo wanasema kuwa walipata zaidi ya maiti mia moja kutokana na shambulizi hilo