ISRAEL: HATUONDOKI GAZA MPAKA TUYAHARIBU MAHANDAKI

Waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu amesema kuwa Israel imeamua kuyaharibu kabisa mahandaki na njia za chini yaardhi zilizojengwa na wapiganaji wa Palestina-Hamas, katika mipaka yake huko Gaza.

Amesema uharibifu huo utatekelezwa na majeshi ya Israeli kukiwa au kutokuwa na muafaka wa kusitisha mapigano.

Netanyahu amesema hayo huku Serikali ya Israel ikishikia kani kuwa kuwa itaendeleza mashambulizi katika eneo la Gaza licha ya shutma za kimataifa kufuatia shambulizi la shule moja ya umoja wa mataifa ambapo takriban watu 15 walipoteza maisha yao.

Msemaji wa serikali ya Israel amesema kuwa wataomba msamaha iwapo watabaini kwamba shambulizi hilo, lilitekelezwa kimakosa na wanajeshi wa Israel.

Umoja wa mataifa umesema kuwa ni wazi kwamba ni jeshila israel ndilo lililorusha kombora hilo katika shule hiyo ambapo zaidi ya raia elfu tatu wa Palestina walikuwa wameomba hifadhi.

Licha ya malalamiko kutoka kote duniani kuhusiana na idadi kubwa ya vifo vyaNjia za chini kwa chini za Hamas ambazo Israeli inalenga kuharibu

Mashambulizi ya Israel kutoka angani na nchi kavu yamerindima kwa milipuko ya mizinga na ndege za kivita.

Na sasa Israel inajiandaa kwavita zaidi baada ya kuwaamuru wanajeshi wa akiba kujiunga na jeshi la taifa. Katika ukanda wa ngazani kilio na majonzi makubwa...