NDEGE YATUA KATIKATI YA BARABARA

Shughuli ziliathirika leo wilayani Mityana baada ya ndege kutua kwa dharura katika barabara ya magari ya Mityana.

Ndege hiyo N604AR, iliyokuwa imewabeba wanajeshi wa Marekani, ilituakatika eneo la Kiwawu umbaliwa kilomita 22 kutoka wilaya ya Mityana.

Kwa mujibu wa mtandao wa Nation, kamishna wa wilaya Joel Walusimbi, alithibitisha tukio hilo akisema rubani wa ndege hiyo alilazimika kutua katikati ya barabara

Polisi walisema kuwa ndege hiyo ilikuwa inaelekea mjini Juba Sudan Kusini kutoka uwanja wa ndege wa Entebbe.