ANYONGA KICHANGA NA KUTUPA KISIMANI

POLISI mkoani hapa inamshikilia msichana wa miaka 18, aliyetajwa kwa jina la Rhoda Idetemya kwa tuhuma ya kumyonga mtoto wake wa miezi miwili.


Ilidaiwa kuwa, Idetemya baada ya kumnyonga mtoto huyo aliyetajwa kwa jina moja la Elizabeth, mwili aliutumbukiza katika kisima cha maji ya kunywa katika Kijiji na Kataya Nyasubi wilayani Kahama.


Ilielezwa kuwa mwili wa mtoto huyo uligundulika katika kisima hicho saa moja jioni wakati mkazi wa eneo hilo Ada Patrick (25) alipokuwa akichota maji.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha alithibitisha kutokea kwa tukio hilona alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliozuka kati ya msichana huyo na baba wa mtoto kukataa kutoa fedha za matumizi ya mtoto.

Chanzo:Habari Leo