AMUUA MTOTO WA MIAKA TISA KISHA KULA UBONGO WAKE

MAUAJI ya kutisha yanaendelea kuuandama mkoa wa Kilimanjaro, baada ya kijana Laurance Flavian (20), mkazi wa Marangu Mashariki kumuua Mwanafunzi wa darasa la Pili katika Shule ya Msingi Marangu Hills, Francis Fortunatus (9), kwa kumkata mapanga sehemu za kichwani na kula ubongo wake, kisha na yeye kujikata uume wake na kusababisha mauaji hayo.


Akizungumza Kamanda wa polisi mkoani humo, Robert Boaz, amesema tukio hilo limetokea leo Ijumaa Julai 18, 2014 saa7:15 asubuhi katika eneo la Marangu Pentekoste katika Wilaya ya Moshi mkoani humo.


Amesema mtoto huyo ambaye pia ni mwanafunzi wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Marangu Hills alikutwa na mauti wakati akielekea shuleni na kuwa kijana huyo (Laurance Flaviani), alianza kumshambulia kwa kumkata na mapanga sehemu za kichwani nakutoa ubongo wake na kuula hali iliyomsababishia, kufariki dunia papo hapo.


Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda Boaz, kijana huyo baada ya kumuua mtoto huyo nayeye alijijeruhi kwa kuukata uume wake, na kukimbizwa katika Hospitali ya Kilema ambapo alikufa wakati akipatiwa matibabu kutokana na kutokwa na damu nyingi kaatika sehemu aliyojikata.

"Mtoto huyu akielekea shuleni asubuhi ghafla kijana huyo ambaye nay eye sasa ni marehemu, alianza kumshambulia kwa kumkata kwa panga kichwani bila sababu yeyote, hali iliyosababisha kifo cha mtoto huyo papo hapo"Kamanda Boaz.

Aidha, amesema chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana na kuwa taarifa za awali kuhusu tukio hilo kinasadikiwa kuwa kijana huyo alikuwa na ugonjwa wa akili na kwamba kabla ya kutenda tukio hilo alikuwa akifanya vurugu na kuvunja vioo vya nyumba yao za watu katika eneo hilo.


Mashuhuda wasimulia

Hata hivyo, taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kijana huyo baada ya kutekeleza mauaji hayo ambapo inadaiwa mtoto aliyemuua ni mtoto wa bosi wake wake na kwamba baada ya kuukata uume wake alianza kuula kama nyama choma huku akikata kipande kimoja baada ya kingine.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Tetrula Kimario, amesema kijana huyo ambaye alikuwa akifanya kazi ya kutengeneza Sanamu za mapambo katika kiwanda kilichopo Marangu Pentekoste, na kuwa Julai 17, 2014 alianza kubadilika kwa kufanya vitu visivyoeleweka ambapo tajiri yake ambaye ni Baba wa mtoto aliyeuawa alimchukua na kumrudisha nyumbani kwao karibu na alipokuwa anaishi mwanzoni.


Amesema, ilipofika leo asubuhi mtoto wa bosi wake alitoka kwenda shule, ndipo kijana huyo alipomkata kichwa na kisha kuanza kula ubongo wake, ambapo watu walifikia katika eneo la tukio waliamua kumpiga kwa mawe hadi polisi walipofika katika eneo la tukio.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, mkoa huo umekumbwa na matukio ya mauaji na unyanyasaji wa watoto waliochini ya umri wa miaka kumi na nane (18).