RAIS WA URUGUAY AWATUKANA MAAFISA WA FIFA

Rais wa Uruguay Jose Mujica amewatukana maafisa wa FIFA kwa kuwaita ''kundi la watoto wa Mbwa'' au "a bunch of old sons of bitches".


Hii ni baada ya maafisa wa shirikisho hilo kumpiga marufuku mchezaji wa nchi hiyo Luis Suarez.

Mchezaji huyo aliitaja adhabuhiyo ya marufuku ya miezi minne ikiwemo kutocheza mechi 19 za kimataifa kama adhabu ya kinazi.


Suarez alipata adhabu hiyo ambayo inasemekana kuwa kali sana kuwahi kutolewa katika historia ya kombe la dunia kwa kumuua mchezaji wa Italia Giorgio Chiellini.


Rais Mujica anasifika kwa kutotafuna maneo yake pamoja na ukali wa matamshi yake.


Aliyatoa matamshi yake kupitia televishini ya taifa alipokuwa anawapokea wachezaji wa timu hiyo baada ya kubanduliwa nje ya michuano ya kombe la dunia katika awamu ya muondoano.


Rais huyo alifunika mdomo wake kwa mshutuko wa kile alichosema , lakini wandishi wa habari tayari walikuwa wamemrekodi.

Pia aliwaambia kuyachapisha matamshi yake alipohojiwa ikiwa alitaka kujirekebisha.


Rais huyo alisema kuwa FIFA ilimuadhibu Suarez kwa sababu ya maisha yake ya zamani ambayo yalikuwa ya unyonge.


Pia alitaja adhabu hiyo kama aibu kubwa sana kwa historiaya FIFA.