MAPIGANO YAENDELEA UWANJA WA NDEGE TRIPOLI

Mapigano yamezuka tena kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Libya, siku mbili baada ya wapiganaji kukubaliana kusitisha mapambano.

Ripoti zinasema kuwa vifaru vinatumiwa katika mapambano makali katika uwanja wa ndege wa Tripoli, ambao umeshambuliwa kwa makombora na mizinga.

Uwanja huo ulianza kushambuliwa juma lilopita na ikalazimika kuufunga.

Wakuu wa Libya wameonya kuwa kazi ya kukarabati uwanja huo itachukua miezi na kugharimu mamilioni ya dola.