MUUZA BANGI AKWEPA JELA, ALIPA FAINI

MUUZA JI wa bangi, Ferdinand Makundi (40) amenusurika kutumikia kifungo cha miaka miwili jela baada kulipa faini ya Sh 100,000 kwa kosa la kukutwa na kilo mbili za bangi.

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama yaWilaya ya Nkasi, mkoani Rukwa, Ramadhani Rugemalira alimhukumu mkazi huyo wa kijiji cha Mkole wilayani humo kutumikia kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya Sh 100,000 baada ya kukiri kosa.

Awali Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi Msaidizi, Hamimu Gwelo alisema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Mei 14 mwaka huu saa 7:00 mchana akiwa nyumbani kwake kijijini Mkole.

Alipotakiwa kujitetea, mshitakiwa aliiomba mahakama hiyo impunguzie adhabu kwa kuwa ana watoto kumi na mke wanaomtegemea.


Chanzo: Habari Leo