WAKAMATWA KWA WIZI WA KILO 40 ZA TANZANITE

WAFANYAKAZI saba wa kampuni yaTanzanite One, wakiwemo viongozi wakuu wa idara ya ulinzi ya kampuni hiyo wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za wizi wa madini aina ya tanzanite yenye uzito wa kilo 40 yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 10.


Akizungumza kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Deusdedit Nsimeki alisema wizi huo ulitokea majira yasaa 8 usiku juzi, ikielezwa wafanyakazi hao walishirikiana na wafanyakazi wa Shirika la Madini laTaifa (STAMICO) kupanga wizi huo.

Nsimeki alisema uchunguzi wa awali umebaini mpango mzima wa viashiria vya upangaji wizi huo umefanywa na wafanyakazi hao na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi ambao bado hawajakamatwa mpaka sasa, lakini polisi iko katika msako mkali dhidi yao.

Alisema kiutaratibu madini yote yanayotoka mgodini kwenda kwenda chumba maalumu cha kuhifadhi madini, husafirishwa na gari maalumu lisiloruhusu risasi kupenya.


Nsimeki alisema cha kushangaza siku ya tukio hilo, shehena hiyo ya madini ilisafirishwa kwa gari ya kawaida aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili T 256 APQ, mali ya kampuni hiyo hatua ambayo ilihisiwa wafanyakazi hao pamoja na viongozi wa idara ya ulinzi walikuwa wanajua kikamilifu kilichokuwa kikiendelea.

Kamanda huyo alisema mara baada ya madini kupakiwa kwenye gari hilo la kupangwa kuelekea katika chumba cha kuhifadhia madini, ghafla walisikia risasi zikilia na moja ya risasi iligonga mlango wa gari hiyo na nyingine kwenye chesisi ya gari.


Kwa mujibu wa kamanda huyo, baada ya walinzi na dereva wa Kampuni ya Tanzanite One kuona hali hiyo nao walitimua mbio bila ya hata ya kujitetea pamoja na kwamba walinzi hao walikuwa na silaha za moto na za kisasa za ulinzi.

''Lakini cha kushangaza muda mfupiwalinzi hao walirejea katika gari nakukuta mifuko miwili ya kilo 15 na 25 imeshachukuliwa na majambazihao na kutoweka nayo,'' alisema.


Hata hivyo, mfuko mmoja wenye uzito wa kilo 25 umepatikana ndani ya gari ya kampuni hiyo, kwani majambazi walishindwa kubeba kwa kuwa ulikuwa mzito nakuchukuliwa na kuhifadhiwa katika ofisi za Tanzanite One.

Nsimeki aliwataja wanaoshikiliwa na polisi ni pamoja na viongozi wakuu wa idara ya ulinzi ambao ni George Odeku Kisambe (38), mkaziwa Arusha ambaye ni meneja wa kitengo cha kamera (CCTV) na pia ni mkuu wa idara ya ulinzi na Jonathan Nyange (52), mkazi wa Kilimanjaro na pia ni dereva wa gari hilo.


Wengine ni Hussein Ng'ombo (64), mkuu wa zamu siku hiyo, Sunday Nzogora (35) mkaguzi wa Madini, Rodney Ngowi (48), na Samwel Kajumu (29) ambao ni mafundi mitambo, wote wakazi wa Mkoa waKigoma na Erick Briygy (44) raia waAfrika Kusini ambaye ni mdhibiti wa madini wa Tanzanite One.

Hii ni mara ya pili kufanyika kwa wizi huo, kwani mara ya mwisho ilikuwa mwaka juzi ambapo watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi walivamia chumba maalumu na kuiba shehena kubwa ya madini yenye thamani ya mabilioni na kutokomea nayo kusikojulikana.