AL SHABAAB WASHAMBULIA TENA LAMU

Kundi la Al shabaab limekiri kutekeleza shambulizi katika basi moja la abiria katika pwani ya Kenya hapo jana usiku.

Shirika la msalaba mwekundu limesema kuwa watu saba walipigwa risasi na kufariki huku wengine wengi wakijeruhiwa.

Shambulizi hilo lilitokea katika mji wa Witu katika Kaunty ya Lamu.

Watu kadhaa wameuawa katika Pwani ya Kenya katika kipindi cha miezi kadhaa iliopita.

Kundi la Alshabaab limekiri kutekeleza mauaji hayo.

Linasema kuwa linalipiza kisasi kuwepo kwa majeshi yaKenya nchini Somali.

Ghasia hizo zimeathiri pakubwa sekta ya utalii nchiniKenya.