409 WAKAMATWA KWA UJANGILI KATAVI

WATU 409 wanaosadikiwa kuwa majangili sugu wamekamatwa wakifanya ujangili katika Hifadhi yaTaifa ya Katavi wilayani Mlele mkoa wa Katavi katika kipindi kilichoanzia Juni 2013 hadi Juni mwaka huu.


Katika kipindi hicho, silaha kadhaa zimekamatwa ndani ya hifadhi hiyoya Taifa zikiwemo bunduki nzito aina ya SMG zipatazo tano, riffle G3 zipatazo nane pamoja na risasi zipatazo 357 za SMG.

Silaha nyingine zilizokamatwa katika kipindi hicho ni pamoja na bunduki aina ya shotgun zipatazo 21, bunduki zilizotengenezwa kienyeji "magobori" yapatayo 138.

Mkuu wa Idara ya Ulinzi wa Hifadhiya Taifa ya Katavi, Mhifadhi Davis Mushi wakati akitoa taarifa katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Mpanda (DDC) iliyoketi mjini hapa.


Alibainisha kuwa kuwepo kwa makazi ya wakimbizi ya Katumba wilayani Mlele na Mishamo wilayani Mpanda karibu na Hifadhi ya Taifa ya Katavi kumesababisha wakimbizi wa makazi hayo kujihusisha ujangili kama njia ya kupatia kipato chao.

Akifafanua alibainisha kuwa mtandao wa watu kupitia mkoa wa jirani wa Kigoma na wakibadilishana na majangili na meno ya tembo.