OBAMA MATATANI, TANZANIA YALAUMIWA

SERIKALI ya Rais wa Marekani, Barrack Obama imeingia lawamani kutokana na kufumbia macho mapigano yanayofanywa nchini Palestina na mamia ya watu wakiangamia, huku wengine wengi wakikosa makazi.

Pia, Serikali ya Tanzania imelaumiwa kukaa kimya katika suala hilo, tofuti na enzi za Hayati Mwalimu Julius Nyerere ambaye alionesha msimamo usioyumba katika kupigania haki za Wapalestina.

Akizungumza Dar es Salaam jana,Balozi wa Palestina nchini Tanzania, Nasri Jaish alisema kinachoendelea Palestina kwa sasa ni mauaji ya halaiki au kimbari(genocide), lakini anashangwa na ukimya wa jumuia ya kimataifa."

Mauaji yanayoendelea Palestina kwa sasa hukuna namna nyingine ya kuyaelezea zaidi ya kusema niya kimbari,kwa kipindi kifupi watu 400 wameuawa,300 kujeruhiwa na nyumba za ibada zimevunjwa.

"Jumuia ya kimataifa, akiwemo Rais Obama anasubiri nini kitokee Palestina ndipo wazungumze, kimsingi inasikitisha. Jumuia ya kimataifa ni lazima ivunje ukimya na kuiambia Israel unyama wanaofanya kwa Wapalestina umetosha,"alisema Balozi Jaish.

Kwa upande wake, Profesa Sheriff Rwizi alisema Tanzania ilikuwa mstari wa mbele kusemea watu wanao kandamizwa, wakiwemo Palestina, lakini anashangazwa na ukimya uliopo hivi sasa.

Akimwelezea Mwalimu Nyerere kuhusu msimamo wake kwa Palestina wakati huo, Profesa Rwizi alifafanua kuwa Mwalimu alisema: "Israel ni lazima iachie maeneo iliyonyakua kutoka kwa Palestina, hakuna anayeweza kuangalia unyonyaji wa aina hiyo ukiendelea," huku akimnukuu Nelson Mandela aliyewahi kusema;

"Ubaguzi ni uhalifu dhidi ya ubinadamu,Israel imewaondoa mamilioni ya watu katika makazi yao, huu ni ukandamizaji mkubwa ambao hauvumiliki."

Kwa sababu hiyo, alihoji iko wapinguvu ya Tanzania leo katika kuwatetea waPalestina.