WHO: WALIOFARIKI NA EBOLA WAFIKA 3000

Shirika la afya duniani limesema kuwa zaidi ya watu elfu tatu sasa wamedaiwa kufariki kutokana na kuzuka kwa ugonjwa wa Ebola katika eneo la Afrika Magharibi kati ya visa elfu sita vya ugonjwa huo vilivyoripotiwa.

Liberia imeathiriwa vibayana ugonjwa huo huku WHO ikisema kuwa kumekuwa na vifo 150 vilivyotokea katika kipindi cha siku mbili pekee.

Idadi hiyo inaweza kupuuzwa kwa kuwa watu wengi wanaogopa kwenda hospitalini.

Hazina ya Fedha duniani IMF imeahidi dola millioni130 kama msaada wa dharura kwa mataifa ya Liberia, Guinea na Sierra Leone.