POLISI WATJA MAJAMBAZI WATANO

Polisi mkoani Kigoma, wamewaua watu watano wanaosadikiwa kuwa majambazi waliokuwa katika harakati za kufanya unyang'anyi wa kutumia silaha kwa kuteka magari ya abiria mkoani humo.

Taarifa hiyo imetolewa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Jafari Mohamed ilisema tukio hilo lilitokea Septemba 3, 2014 saa 11 alfajiri katika pori la Malagarasi Wilaya ya Kasulu.

Kamanda Mohamed alisema polisi imewaua majambazi hao baada ya msako mkali uliotokana na tukio la awali la kutekwa na kulipuliwa kwa bomu basi dogo la abiria aina ya Toyota Hiace lililokuwa likitokea Kata ya Kilelema.

Alisema Agosti 27, walipata taarifa za kuwapo majambazi kutoka nchi jirani ya Burundi wakijiandaa uhalifu.

"Baada ya kupata taarifa, tuliweka mtego katika eneo lililokusudiwa kufanyika uhalifu na muda uliokusudiwa majambazi hao, walifika eneo hilo na walipoona dalili za kukamatwa na askari, walianza kufyatua risasi ovyo na askari wakiwa katika harakati za mapambano waliyaua majambazi hayo," alisema.

Alisema majambazi hao walikutwa na mabomu matatu ya kutupwa kwa mkono.