MABAKI YA MIFUPA YA DINOSAR YAPATIKANA BONDE LA RUKWA

(Picha: Maktaba)


Aina mpya ya dinosaria imetambuliwa kufuatia kupatikana kwa mifupa nchini Tanzania.

Mabaki hayo ya dinosaria yaliyopewa jina la - Rukwatitan Bisepultus - yalipatikana katika korongo moja kwenye eneo la Rukwa(Bonde la Rukwa), kusini magharibi mwa nchi hii.

Inadhaniwa mnyama huyo aliyekuwa akiishi kwa kula majani, aliishi karibu miaka mia moja iliyopita, na alikuwa na uzito sawa na tembo kadhaa na alikuwa na miguu ya mbele yenye urefu wa mita mbili.

Mnyama huyo ni aina ya titanosaurus -- ambao ni wakubwa, na wanao kula nyasi.

Mabaki ya wanyama aina hiyo mpaka sasa yamepatikana katika maeneo ya Amerika ya Kusini, bara ambalo lilijitenga kutoka Afrika katika kipindi cha Cretaceous, (kipindi ambacho miamba ya chaki iliumbika) takriban miaka milioni mia moja na arobaini iliyopita.