MSIKITI WA MASHOGA WAFUNGWA CAPE TOWN

Taj Hargey amekataa kwenda kinyume na mafundisho ya Kiislamu.
Muasisi wa msikiti wa Open Mosque, Taj Hargey ambaye amekataa kwenda kinyume na mafundisho ya Kiislamu.

Msikiti wa kwanza wa mashoga wa nchini Afrika Kusini, ambao unaruhusu wanawake wkuongoza ibada, umefungwa kwa muda usiojulikana, afisa wa hapo aliiambia BBC.


Diwani wa Mji wa Cape Town amesema msikiti huo mpya unaoitwa Open Mosque umevunja sheria za manispaa kwa kutokuwa na sehemu za kuegesha magari.

Msikiti huo ulifungua milango yake rasmi siku ya Ijumaa pamoja na ukosoaji kutoka kwa wanachama wa jumuiya ya Waislamu wa eneo hilo.

Muasisi Taj Hargey aliseme msikiti huo ungesaidia kupambana na imani kali ya kimapinduzi.
“Tunafungua msikiti huu kwa watu wenye mawazo huru, na sio waliofungwa mawazo,” alisema wakati wa ufunguzi.

Diwani wa Jiji Ganief Hendricks alikataa kuwa kufungwa kwa msikiti ni sehemu ya kuwanyanyasa watu wenye mawazo yanayopingana na wengi.