ANUSURIKA MIAKA 30 JELA, AHUKUMIWA VIBOKO

KIJANA wa kiume mwenye umri wa miaka 17, mkazi wa Kijiji cha Karundi wilayani Nkasi katika Mkoawa Rukwa, amenusurika kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka nakumpatia ujauzito msichana mwenye umri wa miaka 16.

Msichana huyo aliyekuwa akisoma darasa la saba alishindwa kufanya mtihani wa Taifa wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika Septemba 10 na 11, mwaka huu.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Nkasi, Ramadhani Rugemalira alisema mshitakiwa mwenyewe baada ya kukiri kutenda kosa hilo, Mahakama hiyo imemtia hatiani chini ya kifungu cha 130 (1) na (2)(e) na 131 (1) cha kanuni ya adhabu Sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Rugemalira aliieleza mahakama hiyo kuwa katika kosa la kwanza la kulawiti, mshitakiwa amehukumiwa kucharazwa viboko 12, na kwa kosa la pili la kumpa ujauzito mwanafunzi huyo atachapwa viboko vinane.

Awali Mwendesha Mashitaka, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Hamimu Gwelo alidai mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo mwaka huu.

Alisema baada ya mwanafunzi huyo kukutwa na ujauzito, mshitakiwa alikamatwa na kufikishwa katika mahakama hiyo kwa kuvunja sheria chini ya kifungucha 130 (1) na (2) (e) na 131 (1) chakanuni ya adhabu Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Aliiomba mahakama hiyo iweze kutoa adhabu kali kwa mtuhumiwa huyo hasa baada ya vitendo hivyo vya ubakaji na kumsababishia ujauzito mwanafunzi ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye nia ya kufanya vitendo hivyo viovu.

Chanzo: Habari Leo