UINGEREZA KUJIUNGA KUISHAMBULIA IS

Uingereza itajiunga na kampeni ya mashambulizi nchini Iraq baada ya wabunge wengi wa taifa hilo kupiga kura za kuunga mkono mashambulizi ya angani dhidi ya wapiganaji wa Jihad kutoka kwa kundi la Islamic state.

Ndege za kijeshi za Uingereza huenda zikajiunga na kampeni hiyo ya mashambulizi wikendi hii.

Wakati wa mjadala huo wadharura katika bunge,waziri mkuu wa UingerezaDavid Cameron alisema kuwa Uingereza ilifaa kuonyesha subra na uvumilivu badala ya mshtuko na hofu katika kukabiliana na tishio linalosababishwa na wapiganaji wa Islamic State.

Bado hakuna uamuzi wa kuongeza mshambulizi ya kijeshi dhidi ya kundi hilo nchini Syria,lakini muhariri wa BBC anayesimamia maswala yakisiasa amesema kuwa Cameron ameonyesha kuwa yuko tayari kuunga mkono hatua kama hiyo.