PSI YAKUTANA NA WAFANYABIASHARA WANAOSAMBAZA KONDOMU MKOA KATAVI


Na khalfani Zozi:

Mwenyekiti wa wafanya biashara Mkoa wa Katavi akifungua kikao.
Jamii wilayani Mpanda mkoani Katavi imetakiwa kuwa na mazoea ya kutumia kondomu ili kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi,mimba zisizotarajiwa sanjari na magonjwa mengine ya zinaa.
Mhamasishaji mkuu wa shirika la PSI Tanzania Kanda ya nyanda za juu kusini Elia Jackson Ndutila.
Mhamasishaji mkuu wa shirika la PSI Tanzania Kanda ya nyanda za juu kusini Elia Jackson Ndutila.
Kauli hiyo imetolewa na muhamasishaji mkuu wa kampuni ya PSI kanda ya nyanda za kusini Jackson Ndutila wakati akizungumza na wasambazaji na wauzaji wa kondomu Mkoani Katavi.

Aidha amesema kuwa jamii isitishike na kuwepo kwa aina nyingi za kondomu kwani zote zina ubora sawa.
Meneja wa Shirika la PSI Tanzania Kanda ya Mbeya,Rukwa na Katavi Bw.Edgar Mchaki.
Naye meneja wa PSI Mbeya, Rukwa na Katavi Edgar Mchaki ameongeza kuwa wananchi mkoani humu wanatakiwa kutumia kondomu ili kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI ambapo imefikia asilimia 5.9 ukilinganisha na asilimia 5.1 kitaifa.
Mganga Mkuu wa hospitali ya Wilaya ya Mpanda Dk.Leonce L.K. Mutajwaha.
Mganga Mkuu wa hospitali ya Wilaya ya Mpanda Dk.Leonce L.K. Mutajwaha.
Kwa upande wake mganga mkuu wa Halimashauri ya mji wa Mpanda Dokta Leonce Mutajwaha amesema kuwa ni wakati wa kila mmoja kuwa mwaminifu kwa mwenza wake ili  kupunguza maambukizi holela ya VVU.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauli ya Mji wa Mpanda Bw.Brian Severe akisoma Risala kwa niaba ya mgeni Rasimi mbele ya wadau wa PSI.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauli ya Mji wa Mpanda Bw.Brian Severe alisema kuwa mchango wa PSI Tanzania umejidhihirisha wazi kutokana na wigo mpana walionao wa usambazaji wa bidhaa za kiafya kwa ajili ya huduma za uzazi wa mpango, kujikinga na maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kujikinga na malaria, kujikinga na magonjwa yanayosababishwa na maji ambayo si salama kwa matumizi ya binadamu, na bidhaa za uzazi wa mpango na uzazi salama kwa akina mama.

Aidha amezitaja bidhaa hizo ikiwa ni pamoja na kondomu za kiume(salama na dume kondomu) water guard, kondomu za wanawake(lady pepeta), vidonge vya uzazi wa mpango, vipandikizi, pamoja na lupu au vitanzi.

Mratibu wa UKIMWI Halmashauli ya Mji wa Mpanda Bi.Mary Byaro akitoa ufafanuzi juu ya kondomu za kike.


Wadau wa bidhaa zinazo sambazwa na PSI Tanzania wakiuliza maswali juu ya matumizi ya kondomu.

Wadau wa bidhaa zinazo sambazwa na PSI Tanzania wakiuliza maswali juu ya matumizi ya kondomu.

Wakala Mkuu wa bidhaa zinazosambazwa na PSI Tanzania akitoa shukulani kwa wadau na wageni waalikwa.