AJALI MBAYA YA BUS YAUA WATU 36 PAPO HAPO

Watu 36 wamefariki dunia papohapo na wengine 79 kujerihiwa vibaya katika ajali mbaya ambayo imetokea saa tano leo asbuhi katika kijiji cha sabasaba nje kidogo ya mji wa musoma wilaya ya butiama mkoani mara kwa kuhusisha mabasi mawili ya abiria na gari dogo aina ya Nissani Tellono yenye namba za usajili T332 AKK.

Mbali na gari hilo kugongwa na kutumbukia ndani ya mto mmoja katika daraja hilo kwenye barabara kuu ya Musoma-Mwanza pia mabasi mawili ambayo yamehusika katika ajali mbaya ni j4 express yenye namba za usali T677 CYC liyokuwa ikitokea jijini Mwanza kwenda sirari wilayani tarime ambalo limegongano uso kwa uso na basi la Mwanza coach yenye namba T736 AWJ lilokuwa likitokea Musoma kwenda jijini Mwanza.

Baada ya taarifa za ajali kusambaa katika manipaa ya musoma vilio na simanzi vimetawala katika mji huo wa Musoma mkoani Mara baada majeruhi na miili ya marehemu wa ajali hiyo kuanza kufikishwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara mjini Musoma.

Wakizungumza wakati wakipatiwa matibabu baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo wamesema kuwa ajali hiyo imesababishwa na mwendo kasi wa mabasi hayo hatua ambayo ilisababisha kushindwa kupishana katika daraja hilo hivyo kugongana uso kwa uso.

Akizungumza kwa niaba ya mganga mkuu wa mkoa wa Mara Dk Martin Khan,amesema kuwa wamepokea maiti na idadi kubwa ya majeruhi na wengi wao hali zao si za kuridhisha.

Hata hivyo Dk Khan ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kujitolea damu kwani amesema kuwa hospital hiyo ya rufaa ya mkoa wa mara inakabiliwa na upungufu mkubwa wa damu katika kuhudimia wagonjwa wakiwemo majeruhi wa ajali.

kamanda wa polisi mkoa wa Mara ACP Alex Kalangi, akizungumza kwa njia ya simu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba taarifa rasmi za jeshi la polisi zitatolewa baada ya kupata taarifa kutoka kwa madaktari na kwamba ametoa wito kwa wananchi kujitokea katika hospitali ya mkoa kwa ajili ya kutambua miili ya marehemu.