AMCHINJA MKEWE MBELE YA WANAE

POLISI mkoani Katavi wanamsaka mkazi wa kijiji cha Urwila wilayani Mlele, Mohamedi Katyukuru (49) kwa kumuua mkewe kwa kumchinja.

Inadaiwa mwanaume huyo alifanyamauaji hayo Septemba 14 mwaka huu wakati watoto wao wawili, wenye umri wa kati ya miaka 11 na14, wakishuhudia.

Inadaiwa baada ya mauaji hayo, alitoroka pamoja na watoto hao na kujificha kusikojulikana.

Alifunga mlango kwa nje na kufanya majirani wachukulie kwamba ametoka kwenda kwenye shughuli zake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alimtaja aliyeuawa kuwa ni Bernadeta Mwetel (38), ambaye mumewe alikuwa akimtuhumu kuwa na uhusiano na mwanamume mwingine.


Chanzo: Habari leo