RAIS JK AWATIMUA MAKADA WALIOENDA KUMPOKEA

Rais Jakaya Kikwete jana aliwafukuza makada wa CCM waliokuwa wakimsubiri kwenye kituo cha dharura cha ebola alipo kitembelea kwa kushtukiza katika Hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Makada hao ambao baadhi yao walivalia sare za CCM, kinyume na matarajio yao, kiongozi huyo alipofika hospitalini hapo alionyesha kuwashangaa kabla ya kuwataka waondoke kwa kuwa hakuhitaji kuzungumza nao, bali wasimamizi wa kituo hicho.

“Hawa watu wote wanafanya nini hapa! Sijajakuhutubia hapa mimi. Ndugu zangu hawa waliowaita wamewasumbua bure, nawashukuruni sana kwa kuja, endeleeni na shughuli zenu,” alisema Rais Kikwete ambaye aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki.

Hatua hiyo ilionekana kuwanyong’onyeza makadahao ambao hawakuwa na jinsi isipokuwa kuondoka taratibu kwenye eneo hilo na kumwacha Rais Kikwete na viongozi wa kituo hicho.

Ukaguzi wa kituo

Katika ukaguzi wa kituo hicho, Rais Kikwete alielezakutoridhishwa na maandalizi na akaagiza ukarabati mkubwa ufanywe haraka ili kiwe na hadhi inayostahili.

Alionyesha kushangazwa na miundombinu duni ikiwamo vyoo vibovu na ukosefu wa maji katika kituo hicho na kuagiza kufanyika marekebisho ya haraka.

“Hivi hii ni kweli? Hakuna maji, vyoo vibovu, kituo chenyewe kikuukuu! Kwa taarifa za awali, kituo hiki kilikuwa ni kwa ajili ya ugonjwa wa kipindupindu, hakiendani kabisa na hitajila sasa la kuwa hudumia wagonjwa wa ebola iwapo watabainika kuingia nchini,” alisema Rais Kikwete.

Alisema katika hali ya kawaida, kituo hicho kinatakiwa kuwa cha kisasana chenye mazingira yanayowezesha kutoa huduma kwa wagonjwa hao kwa usalama.

Alisema ameamua kufanyaziara hiyo Temeke na ukaguzi wa namna Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kuona ukweli wa taarifa alizopewana kuzizungumza katika mkutano na wazee wa Mkoa wa Dodoma wiki iliyopita.

“Hii ndiyo fursa ya hii dharura ambayo mnatakiwa kuitumia vyemana kupata kituo cha kisasa na kwa wakati huu. Kama kuna matatizo ya fedha tuelezane tutajua namna ya kufanya,” alisema Rais Kikwete.

Alisema ni vyema kuhakikisha kunakuwa na kituo maalumu cha kuwapokea na kuwahifadhi waathirika wa magonjwa ya mlipuko ambacho ni cha kipekee na cha aina yake nchini.