OBAMA: TULIKOSEA KUKADILIA NGUVU YA IS

Rais Obama amekiri katika televishen ya kitaifa kuwa Mashirika ya Marekani yalikosea katika kukadiria hatari ya wapiganaji wa dola ya kiislam, Islamic State nchini Iraq na Syria.

Amesema kuwa wapiganaji hao wenye uhusiano na Al Qaeda walitumia fursa ya kutokuwepo serikali thabiti nchini Syria na kuongezewa nguvu zaidi na vijana waliojiunga kupigania jihadi kutoka mataifa mengine.

Hata hivyo Obama amesema wapiganaji hao waliwahi kuvurumishwa huko Iraq na majeshi ya nchi yake yakishirikiana na kabila la Sunni.

Obama amekiri vyombo vya Ujasusi vya Marekani zilikadiria vibaya uwezo wa majeshi ya Iraq kupambana na wapiganajiwa kiislamu ambao wameteka maeneo mengi nchini humo.