IDADI YA WATU WANAOJIUA YAONGEZEKA DUNIANI

Shirika la afya ulimwenguni WHO limetowa ripoti yake inayosema kwamba idadi ya watu wanaojiua duniani imeongezeka na kufikia kiwango cha kutishaRipoti inasema kwamba katika kila sekunde 40 mtu mmoja anajiua.

Shirika hilo limelitaja tatizo hilo kama la kiafya ambalo linahitaji kushughulikiwa baada ya kufanya utafiti wake katika nchi 172 duniani.

Barani Afrika nchi zilizotajwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaojiua ni Msumbiji,Tanzania,Burundi Sudan Kusini na Uganda.

Tanzania iko katika nafasi ya pili barani Afrika ikiwa na asilimia 24.9 ya vifo hivyo vya kukusudia.