MWANDISHI MWINGINE ACHINJWA, OBAMA AONGEZA WANAJESHI

Wapiganaji wa dola ya Kiislam IS wamesambaza picha za video katika mitandao kwa lengo la kuonyesha kuchinjwa kwa mwandishi wa habari raia Marekani Steven Sotloff ambaye ni mmoja wa mateka wanaoshikiliwa na wapiganaji hao.

Mwandishi huyo Sotloff, mwenye umri wa miaka 31 ambaye alitekwa na wapiganaji hao mwezi August mwaka jana.

Mwezi uliopita Sotloff alionekana mwishoni katika picha za video zilizoonyeshwa kuhusiana na kuchinjwa kwa mwandishi mwingine wa Marekani James Foley.

Wapiganaji hao wa katika picha hizo pia wameonekana wakimtishia kumuua mateka mwingine anayedhaniwa kuwa ni raia wa Uingereza.

Baada ya mauaji ya mwandishi wa awali Foley, mama mzazi wa mwandishi wa Sotloff alitoa ombi maalumu kwa kiongozi wa wanajeshi hao Abu Bakr al-Baghdadi kutoa muua mtoto wake.

Msemaji wa Ikulu ya White House Josh Earnest amesema kuwa maofisa wa Marekani wanaendelea na uchunguzi wa ripoti hiyo.

Marekani hivi karibuni ilifanya mashambulizi ya anga dhidi ya IS nchini Iraq.

Mwandishi wa masuala ya usalama wa BBC Frank Gardner amesema hatua hiyo ya wapiganaji wa IS ni kulipa kisasi kwa Marekani.


OBAMA AIDHINISHA WANAJESHI KUONGEZWA

Rais Barack Obama wa Marekani ameidhinisha kupelekwa vikosi vya wanajeshi wapatao 350 kwa lengo la kuwalinda wanadiplomasia na wafanyakazi raia wa nchi hiyo waishio mji mkuu waIraq Baghdad.

Ikulu ya Marekani imesema wanajeshi hao watakaopelekwa baadhi yao ni wale wanaojihusisha na diplomasia ya ulinzi ya iraq ambao ni zaidi ya mia nane.

Hata hivyo Marekani inatarajia kuwatuma maofisa waandamizi akiwemo John kerry katibu mkuu wa marekani na Chuck Hagel katibu wa ulinzi ambao watakwenda mashariki yakati katika harakati za kuimarisha ushirikiano.

Hatua hiyo inafuatia vitendo vya mashambulizi na mauaji yanayoendelea Iraq ikiwani matokeo ya utofauti kati ya Marekani na makundi ya wapiganaji ambao wamekuwa wakiwalenga raia wa Marekani waliopo nchini humo.