POLISI 6 WAUAWA KATIKA MLIPUKO

Askari polisi 6 wameuawa katika mlipuko katika rasi ya Sinai Misri wizara ya maswala ya ndani ya Misri imetangaza.

Polisi hao waliuawa bomu lililokuwa limetegwa kando ya barabara ilipolipuka msafara wa polisi ukipita.

Maafisa wawili zaidi walijeruhiwa vibaya katika tukio hilo.

Wanamgambo katika rasi ya Sinai wameendeleza mashambulizi zaidi haswa baada ya kung'olewa mamlakani kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Mohammed Morsi mwaka uliopita.

Shambulizi hili la leo lilitokea katika barabara ya kutoka mji wa rafah Kuelekea mpaka wa Palestina wa Gaza.

Kundi la wapiganji wa Ansar Beit al-Maqdis wanaohusishwa na Al Qaeda ndio waliodai kutekeleza shambulizi hilo.

Kundi hilo linadai kulipiza kisasi mauaji ya maelfu ya waislamu waliouawa katika mapinduzi ya Morsi.