AUWAWA NA MWILI KUTUPWA KISIMANI

MWANAKIJIJI cha Itenka Tarafa ya Nsimbo wilayani Mlele Katavi, Mary Magese (39) ameuwawa na mwili wake kutupwa katika kisima cha maji.

Mauaji hayo yalifanyika Septemba 14 mwaka huu saa mbili usiku kijijini hapo baada ya marehemu kumaliza kula chakula cha usiku akiwa na mume wake Lazaro Maziku (40).

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema wanandoa hao walipomaliza kula mume alikwenda bafuni kuoga.

Aliporudi hakumkuta mkewe hivyo alianza kumtafuta bila mafanikio ndipo alipokwenda kwa majirani na ndugu zake pia hakumpata.

Alisema siku iliyofuata saa mbili asubuhi zililizagaa taarifa ya kuwpeo kwa maiti kisimani ndipo uongozi wa kijiji ulipokwenda na kuukuta mwili wa mke wa Maziku Kidavashari alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi kati ya Maziku na Shija Joseph aliyetuhumiwa kuwa hawara wa marehemu kwa muda mrefu.

Alisema jeshi la polisi linamshikilia mume wa marehemu kuhusiana na kifo hicho kwa mahijiano zaidi na atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kumekamilika.

Chanzo:Tz Daima