POLISI KUCHUNGUZA LUGHA ZA KIBAGUZI DHIDI YA BALOTELLI

(Picha: Tweets za kibaguzi dhidi ya Balotelli)

Mario Balotelli alipokea ujumbe wa kibaguzi baada ya kutuma ujumbe kwenye Twitter kwenye mechi ya Man United iliyofungwa 5-3 na Leicester siku ya Jumapili.
Raia huyo wa Italia alipokea udhalilishaji huo baada ya kutuma ujumbe 'Man Utd…LOL'wakati wa kipigo cha kushtukiza kutoka Leicester siku ya Jumapili.
Nyota huyo, 24, alijibiwa zaidi ya mara 150,000 na kukutana na mfululizo wa wabaguzi na jumbe za matusi.
Baadhi ya akaunti zilizotuma jumbe za matusi zimeshafungiwa.
Polisi wanasema kwanza watahitaji kumjua nani alituma jumbe hizo na kujua alitoka wapi.
Kundi linalopambana na ubaguzi la Kick It Out lilisema watumiaji wa mitandao ya kijamii walitahadharisha hili kwa jumbe ya kibaguzi iliyotumwa kwa mchezaji wa zamani wa Manchester City.
"Tunaendelea kutoa msaada wetu kwa Mario Balotelli baadaya udhalilishaji wa kibaguzi kuelekezwa kwake," alisema msemaji.