MSHIKAMANO ARTS WAFANYA USAFI

Vijana wa kikundi cha MSHIKAMANO ARTS GROUP cha mjini Mpanda Waanzisha kampeni ya usafi katika Mji huo(MPANDA) ijulikanayo kwa jina la "USAFI WA MJI NI MIMI NA WEWE".

Kampeni hiyo ambayo pia inashirikisha wasanii wa kundi la muziki wa kizazi kipya KATAVI FOR REALY itakua ikifanyika kila siku ya jumamosi ili kudumisha hali ya usafi mjini kwa kila mtu kufanya usafi eneo lake la kazi na mazingira yanayomzunguka.

Sambamba na hayo kutakuwa na uzinduzi wa kampeni hiyo tarehe 12/10/2013 katika viwanja vya kashaulili, uzinduzi utakaoambatana na burudani ya muziki na michezo ya jukwaani toka makundi hayo ya sanaa.


Picha:Majaliwa Rubuye