JAMAA ACHARAZWA MBOKO HADHARANI

JAMAA mmoja ameonja joto
ya jiwe baada ya kucharazwa
bakora 100 hadharani kama
adhabu baada ya kufanya
uasherati.


Mtu huyo ambaye hajaoa,
aliyetambuliwa kwa jina
moja la Mallam mkazi wa
Jimbo la Borno nchini
Nigeria alipata mkong'oto
huo baada ya kulala na
msichana asiyeolewa.


Mallam alipewa adhabu hiyo
kwa vile vitendo vya ngono
kabla ya ndoa (uasherati) ni
mwiko hivyo vinapigwa vita
katika jamii hiyo.