MWANAUME KWENYE KORODANI NDOGO ANAUWEZO KUJALI FAMILIA KULIKO MWENYE KORODANI KUBWA

Wanasayansi wanasema
kuwa kuna uhusiano kati ya
ukubwa au udogo wa
Korodani (Testicles) za baba
na uwezo wa baba
kutekeleza majukumu yake
kama mzazi wa watoto wao.

Watafiti katika chuo kikuu
cha Emory nchini Marekani,
wanasema kuwa wanaume
walio na Korodani ndogo
huenda wakayachukualia
majukumu yao kwa uzito na
hata kujihusisha na
kumbadilisha mtoto nepi,
kumlisha na hata
kumuogesha mtoto.

Pia uligundua kuwa utofauti
katika picha ya ubongo wa
baba wakitizama picha za
waoto wao, ilihusishwa na
ukubwa au udogo wa
Korodani.

Lakini mambo mengine ya
kitamaduni yanaweza
kuchangia kwenye uhusiano
kati ya Korodani na
majukumu ya baba kwa
mwanawe.

Uasherati na ukubwa wa
korodani zinajulikamna
kuwa na uhusiano mkubwa
kwa wanyama , wale walio
Korodani kubwa hujamiiana
na wanyama wengi kinyume
na walio na Korodonani
ndogo.

Watafiti walikuwa
wanachunguza nadharia
kuhusu ikiwa wanaume
hutumia muda zaidi katika
kuwa na mahusiano ya
kimapenzi au kulea watoto
wao. Wazo lao likiwa
kwamba wanaume walio na
Korodani kubwa hutumia
muda wao katika kuzaa
watoto wengi kuliko katika
kuwalea watoto hao.

Utafiti huo ulichunguza
uhusiano kati ya ukubwa wa
Korodani na mfumo wa
uzazi katika wananume 70
waliokuwa na watoto walio
kati ya umri wa mwaka
mmoja na miwili.
Watafiti waliwapiga
wanaume hao picha ya
ubongo wakiwa wanatizama
picha za wanao.

Utafiti wao ulionyesha kuwa
wanaume wenye Korodani
ndogo walionekana kuwa
makini katika malezi kuliko
wale wenye kubwa.

Wale waliokuwa na
Korodani ndogo
walionekana kuwa na wazazi
wazuri wanaojihusisha na
kubadilisha mtoto nepi na
kumuogesha, yaani
alijihusisha vyema katika
majukumu ya mzazi.
Mmoja wa watafiti alisema
kuwa uchunguzi wao
unaonyesha kwamba kuna
baadhi ya wanaume ambao
ni wazazi wazuri tu na
ambao wanajihusisha na
majukumu ya ulezi kuliko
wengine.

Watafiti hao waliona kuwa
ukubwa au udogo wa
Korodani unaweza kuathiri
tabia za mtu, lakini
haijulikani kama hatua ya
kumpata mtoto hubadili
mawazo na mienendo ya
baba.