KATAVI WACHEZEA KICHAPO TOKA RUKWA

Rukwa imeanza vizuri michuanoya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 baada ya leo kuichapa Katavi mabao 4-0 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Shule yaSekondari Iyunga jijini Mbeya.

Mabao ya washindi yalitiwa wavuni na Tumaini Boniface dakika ya 13 na 65, Francisco Mkanga akipachika la pili dakika ya 29 wakati la mwisho lilifungwa dakika ya 75 na Innocent Ahombile.

Katika kituo cha Zanzibar, wenyeji Mjini Magharibi imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kaskazini Pemba kwa mabao ya Faisal Salum na Masoud Mohamed.

Mechi ya pili katika kituo hicho ilikuwa kati ya Kusini Pemba na Kusini Unguja. Bao pekee lililofungwa na Othman Abdallah lilitosha kuipa ushindi wa 1-0 timu ya Kusini Pemba.