KUMI BORA AFRIKA WAPANGWA

MABINGWA wa soka wa
Afrika, Nigeria
wamepangwa na timu
isiyopewa nafasi sana,
Ethiopia, wakati Ghana
imekabidhiwa shughuli
pevu mbele ya Misri katika
mechi za mchujo za
kusaka tiketi ya fainali za
Kombe la Dunia
zitakazofanyika mwakani
Brazil.

Droo ya mechi hizo
imefanyika muda mfupi
uliopita
Ivory Coast vs Senegal,
Ethiopia vs Nigeria,
Tunisia vs Cameroon,
Ghana vs Misri, Burkina
Faso vs Algeria. Mechi za
kwanza za mchujo huo
zinatarajia kufanyika kati
ya Oktoba 11 na 15, wakati
marudiano zitakuwa kati
ya Novemba 15 na 19
mwaka huu.