AL SHABAAB WASHAMBULIA TENA

Al-Shabaab leo imevamia tena kituo cha polisi katika mji mdogo wa Mandera uliopo mpakani mwa Kenya na Somalia na kuua polisi wawili na wengine kujeruhiwa kisha kuchoma moto magari 11. Duru za uchunguzi zinaonesha hii ni sehemu tu ya mfulululizo wa mashambulizi waliyoyaandaa.