LUKUVI KUFANYA ZIARA KATAVI, MBEYA NA RUKWA

Waziri wa Nchi Ofisi ya
Waziri Mkuu (Sera
Uratibu na Bunge) Mhe.
William V. Lukuvi (MB)
kuanza ziara rasmi leo
tarehe 16 hadi 19
Septemba, 2013 katika
Mikoa ya Katavi, Rukwa
na Mbeya.

Katika ziara hiyo Waziri
Lukuvi anatarajiwa
kutembelea baadhi ya
vituo vya Ununuzi wa
Mahindi kwa ajili ya
kuhifadhiwa kwenye
Maghala ya National
Food Reserve Agency
(NFRA), Maghala ya
NFRA ya kuhifadhi
chakula, atapokea
taarifa ya Utekelezaji
kuhusu Mradi wa
Miundo Mbinu ya
Masoko na Uongezaji wa
Thamani (MIVARF)
katika maeneo
yanayotekeleza mradi
huu.


Vilevile Mhe. Lukuvi
atapokea Taarifa ya
Utekelezaji wa Miradi
yote ya Maendeleo
ikiwemo Miradi
itokanayo na ahadi za
Mhe. Rais na Miradi
itokanayo na Ilani ya
Chama Tawala pamoja
na Miradi
inayofadhiliwa na
Taasisi mbalimbali
Mkoani humo.