Kaimu katibu mtendaji wa baraza la mitihani, Charles Msonde amesema jumla ya watahiniwa 427,606 kati ya 844,938 wamefaulu mtihani kwa kupata alama zaidi ya 100 katika jumla ya alama 250.
Watahiniwa wamefaulu zaidi somo la kiswahili kwa asilimia 69.06 na somo ambalo wamefaulu kwa kiwango cha chini ni hisabati maana ufaulu wake ni asilimia 28.62