AMUUWA MJUKUU WAKE KWA KUMPIGA NA FIMBO KICHWANI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linamshikila Zenobi Lusale (65) Mkazi wa Kijiji cha Sibwesa Tarafa ya Karema Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumuuwa mjukuu wake kwa kumpiga na fimbo kichwani.

Baada ya kumtuhumu kumwibia debe moja la mahindi Kwa mujibu wa Kaimu kamanda wa polisi wa Mkoa wa Katavi Joseph Shilinde tukio hilo lilitokea majira ya saa kumi na moja jioni katika kitongoji cha senta Magogo Kijiji cha Simbwesa Tarafa ya Karema Wilayani hapa.

Kaimu kamanda Joseph Shilinde alimtaja aliyeuwawa kwa kupigwa na fimbo kichwani na babu yake kuwa ni Stansilaus Joseph (15) Mkazi wa kijiji hicho.

Siku hiyo ya tukio mtuhumiwa Zenobi alikwenda kwa jirani kunywa pombe ya kienyeji aina ya komoni mida ya mchana na kisha aliporejea nyumbani kwake aliko kuwa akiishi na mjuu kuu wake huyo na ndipo alipo mwita kwa lengo la maongezi.

Marehemu aliitika wito huo wa Babu yake kwa kujua wanataka kufanya mazungumzo kama ambavyo wamekuwa wakifanya yeye na Babu yake mara kwa mara.

Kaimu Kamanda alieleza kuwa ndipo mtuhumiwa alipoanza kumshutumu marehemu mjukuu wake kuwa kuna mahindi debe moja yameibiwa ndani na yeye marehemu ndiye aliyeiba mahindi hayo.

Marehemu baada ya kuambiwa tuhuma hizo alimkatalia katakata Babu yake kuwa yeye haja iba mahindi hayo labda aliuza mwenyewe na amesahau kama alimuuzia mtu kwani yeye hana tabia ya wizi.

Mtuhumiwa baada ya kujibiwa hivyo na marehemu alianza kumshambulia kwa fimbo kichwani huku mjukuu wake huyo akipiga mayowe na ya kuomba msaada na huku akimsihi babu yake asiendelee kumpiga lakini hakufanya hivyo aliendelea kumpa kichapo tuu.

Majirani walifika katika eneo hilo na kumkuta mtuhumiwa akiwa ameshika fimbo hiyo aliyotumia huku marehemu akiwa amegalagala chini na huku akiwa ameishafariki dunia kutokana na kipigo hicho na majirani hao walimkamata mtuhumiwa na kumweka chini ya ulinzi.

Polisi walifika kwenye eneo hilo na kumkuta mtuhumiwa akiwa chini ya ulinzi wa wanakijiji hicho na ndipo walipomchukua hadi katika kituo cha polisi cha Mpanda Mjini.

Shilinde alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospital ya Wilaya hii na mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara uchunguziwa tukio hili utakapo kuwa umekamilika.


Chanzo:Katavi Yetu Blog