KIZIMBANI KWA KUKOJOLEA QURAN

Mtu mmoja Mkazi wa Nsemulwa Kichangani mjini Mpanda Mkoa wa Katavi Jafeti Nobeti (15) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mfawidhi mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Chiganga Ntengwe kwa tuhuma za kukojolea Quran Tukufu.

Mtuhumiwa anadaiwa kutenda kosa hilo majira ya saa tano asubuhi katika eneo la msiki wa Kichangani uliopo katika mtaa wa Nsemlwa mjini hapa.

Mwanasheria wa Serikali wa Mkoa wa Katavi Mwandolomi aliileza Mahakama kuwa siku hiyo ya tukio mtuhumiwa alikojolea Quran hiyo ambayo ilikuwa imewekwa na watoto wa kisramu ambao walikuwa wakisoma madrasa iliyoko katika msikiti huo.

Ilielezwa wakati watoto wa madrasa wakiendelea na mchezo wa mpira wa miguu wakati wa kipindi cha mapumziko ndipo mtuhumiwa Jafeti alipofika kwenye eneo hilo akitokea kwao ambapo ni jirani na msikiti huo.

Watoto wa Madrasa wakati wakiendelea na mchezo wa mpira ndipo walipo mwona mtuhumiwa akiwa anakojolea Quran hiyo hari ambayo iliwashitua na kumfuata mtuhumiwa na kuanza kumshambulia kwa kipigo.

Mtuhumiwa aliendelea kupokea kipigo hadi hapo alipokuja kuokolewa na mwalimu wa Madrasa hiyo Ustadh Khalfan Juma na Shekhe wa mtaa Shekhe Yusuph Mkumba ambao walilazimika kumuhifadhi kwenye nyumba ya mwalimu wa madrasa hiyo na baada ya hali kuwa tulivu walimpeleka kwenye nyumba ya mwalimu huyo na kisha hali ilipokuwa shwari walimpeleka kwenye kituo cha polisi cha mpanda mjini.

Mtuhumiwa baada ya kusomewa mashtaka alikiri kutenda kosa hilo lakini alieleza kuwa hakufanya kitendo hicho kwa maksudi bali wakati alipokua akikojolea hakujua kama ni Quran alidhani kuwa ni kashala kuhifadhia kanda za video hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya mpanda Chiganga Ntengwa baada ya mtuhumiwa kusomewa mashtaka na kukirikutenda kosa hilo bila kukusudia aliahirisha kesi hiyo hadi hapo Nov 14 hata hivyo mtuhumiwa aliweza kupata dhamana baada ya kutimiza masharti ambapo alitakiwa adhaminiwe na mtu mmoja kwa dhamana ya shilingi milioni moja na nusu kwani hakimu Chiganga kutokana na umri wa mtuhumiwa kuwa mdogo isingekuwa busara kwa mtuhumiwa kupelekwa mahabusu.


Chanzo: Katavi Yetu Blog