BABU SEYA NA PAPI KUENDELEA KUKAA JELA RUFAA YAO YATUPILIWA MBALI

Mahakama, nchini Tanzania imetupilia mbali ombi la kusikilizwa upya kwa kesi dhidi ya muimbaji Nguza Viking, anayejulikana kama Babu Seya pamoja na mwanawe, ambao walihukumiwa maisha jela, kwa kosa la ubakaji.

Majaji walisema kua kuna thibitisho tosha kuwa wawili hao waliwabaka watoto 10 wa shule ya msingi mwaka 2013.

Katika kesi yao ya kwanza ya rufaa miaka mitatu iliyopita, watoto wengine wawili wa muimbaji huyo, ambao pia walipatikana na hatia ya kosa hilo mwaka 2004, waliachiliwa.

Kesi hiyo imewashtua mashabiki waViking katika nchi hiyo iliyo katika kanda nzima ya Afrika Mashariki.

Mwanamuziki huyo mwenye kuimba nyimbo za Rhumba, ambaye ni mzaliwa wa DRC, ameishi Tanzania kwa miaka mingi na kuwa na ufuasi mkubwa huko.

Viking na kijana wake Johnson Nguza ambaye pia ni mwanamuziki,walifika mahakamani kwa uamuzi huo.

Walionekana kuwa watulivu wakati majaji walipotupilia mbali ombi lao kutaka hukumu yao kubatilishwa.

Walihukumiwa kwa kuwabaka wasichana 10 wa shule ya msingi waliokuwa kati ya umri wa miaka sita na nane wote waliokuwa katika shule ya msingi ya Mashujaa mtaaniKinondoni mjini Dar es Salaam.

Wakili wa muimbaji huyo alisema kua muimbaji huyo hana matumaini tena ya kupewa rufaa kwani hili ndio lilikuwa ombi lake la mwisho.