DAKTARI AKAMATWA AKITAKA KUMTOA MIMBA BINTI

Polisi mkoani Kilimanjaro, imemtia mbaroni daktari mstaafu wa Hospitali ya Serikali ya Mkoa ya Mawenzi kwa tuhuma za kumtoa mimba msichana wa miaka 17.

Tukio hilo linadaiwa kutokea juzi, ambapo Dk huyo anayedaiwa kuwa na umri wa miaka 50 (jina tunalo), alikamatwa saa 10:45 alasiri katika nyumba ya mjomba wake iliyopo eneo la Kiboriloni mjini hapa akiwakatika harakati za kufanya tukio hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz aliwaambia wanahabari jana kuwa, uchunguzi umebaini msichana aliyekuwa akitolewa mimba ni mhitimu wa Chuo cha Ualimu Masama Suni.

Kwa mujibu wa Kamanda Boaz, msichana huyo amelazwa katika Hospitali ya Mawenzi akiendelea kupatiwa matibabu baada ya jaribio hilo la kumtoa mimba kuzimwa na polisi kabla halijakamilika.

Katika tukio kama hilo, daktari mmoja aliwahi kumsahau mwanafunzi aliyekuwa akimtoa mimba na kwenda kunywa pombe na baadaye mwanafunzi huyo alipoteza maisha.

Desemba 20,2012 Polisi lilimtia mbaroni daktari bingwa wa magonjwa ya akina mama pia.