JK MGENI RASMI ZIARA YA KOMBE LA DUNIA

Kombe halisi la Dunia la Shirikisho la Soka la Dunia(FIFA) litawasili nchini Novemba 29 mwaka huu ikiwa ni sehemu ya ziara yake katika nchi 88 duniani kote.

Akizungumza wakati wa hafla ya kutangaza ujio wa kombe hilo, Meneja Mkazi wa Coca-Cola Tanzania inayodhamini ziara hiyo, Yebeltal Getachew alisema, Novemba 30 maelfu ya mashabiki wa soka watapata fursa ya kulishuhudia kombe hilo katika tukio litakaofanyika kwenye Uwanjawa Taifa, Dar es Salaam.

Getachew alisema,mgeni rasmi wakati wa ziara ya kombe hilo hapanchini atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.

"Wito wangu kwa mashabiki wa soka hususani wa Dar es Salaam wajitokeze kwa wingi wakati wa ujiowa kombe hilo hasa kutambua kwamba hii ni fursa adimu,"alisemaGetachew na kuongeza:

"Mashabiki watapata fursa ya kupiga picha, kutazama video zinazoonyesha matukio mbalimbaliya kihistoria ya Kombe la Dunia la FIFA na kufurahia burudani za kusisimua.

"Alisema, ujio wa kombe hilo kwa mwaka huu 2013, umezingatia mafanikio ya ziara zingine za Kombe Halisi la FIFA zilizowahi kufanyika mwaka 2006 na 2009.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Michezo, Leonard Thadeo alisema, ziara hiyo itasaidia kuitangaza Tanzania katika medani ya kimataifa.

"Mkumbuke kwamba ujio wa Kombe la Dunia hapa nchini utaambata na vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa hivyo ni wazi sisi kama nchi tutapata nafasi ya kujitangaza kimataifa,"alisema Thadeo.